Page 38 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 38

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari




             Somo la 7:  Kutathmini mchango wa nadharia teule za uhakiki
                        wa kazi  za  fasihi katika maendeleo  ya ushairi na
                        tamthiliya
           FOR ONLINE READING ONLY
           Shughuli ya 3.17

           Hatua za ufundishaji

              (i)  Waongoze wanafunzi kukaa katika  vikundi visivyozidi
                  wanafunzi sita ili kufanya shughuli ya 3.17 iliyomo kwenye
                  Kitabu  cha  Mwanafunzi  kisha kuwasilisha  kazi  zao darasani
                  kwa majadiliano zaidi huku ukirekebisha upungufu unaojitokeza
                  wakati wa majadiliano ili kuleta uelewa wa pamoja.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 3.17 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
           shughuli hii, mwanafunzi atachagua utanzu wa ushairi au tamthiliya,
           kisha  kueleza  namna  nadharia  za  umaksi  na  mwingilianomatini
           zinavyochangia katika maendeleo na uhakiki wa tanzu hizo.

              (i)  Waelekeze wanafunzi kukaa katika jozi ili kufanya zoezi la 3.4
                  lililomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha kusanya kazi za
                  wanafunzi, sahihisha na kutoa mrejesho.

              (ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi kufanya maswali ya
                  tamrini yaliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

              (iii) Sahihisha na toa mrejesho kuhusiana na shughuli husika kwa
                  wakati.

           Majibu

           Majibu ya zoezi la 3.4 na maswali ya tamrini yatatokana na uelewa wa
           mwanafunzi. Mwanafunzi ajibu kulingana na mahitaji ya swali husika.
           Pia, hakikisha mwanafunzi anahusisha maarifa na maisha yake ya kila
           siku.


             32                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   32    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   32
   33   34   35   36   37   38   39   40   41   42   43