Page 34 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 34
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
hakikisha kila mwanafunzi anashiriki katika uwasilishaji.
Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.
Majibu
FOR ONLINE READING ONLY
Majibu ya shughuli ya 3.11 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze maana na misingi ya nadharia
ya mwingilianomatini katika kuhakiki kazi za kifasihi.
Shughuli ya 3.12
Hatua za ufundishaji
(i) Tumia mbinu ya fikiri-jozisha-shirikisha, kisha waongoze
wanafunzi kufikiri, kisha waelezane mawazo yao katika jozi.
Baada ya kuyaunganisha mawazo ya jozi, kila jozi iwasilishe
mawazo yao darasani.
(ii) Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji wa
majibu ya shughuli ya 3.12.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 3.12 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze kwa mifano sifa na dhima
za mhakiki wa kazi za kifasihi. Pia, mwanafunzi aoneshe athari hasi
za kutokuwa na mhakiki wa kazi za kifasihi ili kupata mitazamo
mbalimbali.
(i) Waelekeze wanafunzi kufanya zoezi la 3.2 lililomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, kisha kusanya, sahihisha na toa
mrejesho.
28 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 28
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 28 23/06/2024 17:48