Page 30 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 30
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
kawaida kwa kuchunguza mifano na uelezwaji wa hoja kwa kila swali.
Pia, hakikisha mwanafunzi anazingatia mahitaji ya kila swali.
Somo la 4: Nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi
FOR ONLINE READING ONLY
Shughuli ya 3.4
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kubungua bongo kuhusu maana na sifa za
nadharia za uhakiki, kisha wajibu maswali hayo.
(ii) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi, kisha watumie
vyanzo vya mtandaoni na maktabani kujadili shughuli ya 3.4
iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha waliyoyajadili, kisha
hitimisha kwa kuwapa maelezo sahihi kuhusiana na nadharia za
uhakiki wa kazi za fasihi. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki
kikamilifu.
(iv) Unashauriwa kukazia maarifa kwa sababu uhakiki wa kutumia
nadharia haujazoeleka sana kama ule wa uchambuzi wa fani na
maudhui.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 3.4 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze maana, sifa na umuhimu wa
nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi. Hakikisha mwanafunzi anaeleza
bayana vipengele hivyo.
24 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 24
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 24 23/06/2024 17:48