Page 26 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 26
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Sura ya
Tatu Kutathmini kazi za fasihi
FOR ONLINE READING ONLY
Utangulizi
Katika sura hii, mwanafunzi atajifunza kuhusu mitazamo, uhusiano
na umuhimu wa vipengele vya fani na maudhui katika kazi za fasihi.
Pia, atajifunza nadharia za uchambuzi wa kazi za fasihi pamoja na
kuzitumia katika kuchambua kazi mbalimbali za kifasihi. Baada ya
kujifunza ataweza kukuza stadi za uandishi na uchambuzi wa kazi za
kifasihi. Mwalimu utapata baadhi ya mbinu zilizopendekezwa ambazo
zitakuwezesha katika ujenzi wa umahiri huu kwa mwanafunzi. Hata
hivyo, unashauriwa kutumia mbinu nyingine utakazoona zinafaa
kulingana na mazingira yako ili kukamilisha shughuli husika.
Shughuli za kutendwa na mwanafunzi
(a) Kujadili mitazamo inayohusu fani na maudhui;
(b) Kuhusianisha fani na maudhui katika kazi za fasihi;
(c) Kueleza umuhimu wa vipengele vya fani na maudhui katika
kazi za fasihi;
(d) Kuchambua nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi;
(e) Kuhakiki kazi za fasihi kwa kutumia misingi na nadharia
mbalimbali; na
(f) Kutathmini mchango wa nadharia za uhakiki katika maende-
leo ya ushairi na tamthiliya.
20 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 20 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 20