Page 24 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 24

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari



             Somo la 5:  Mchango wa fasihi simulizi na fasihi andishi katika
                        maendeleo ya jamii


           Shughuli ya 2.19
           FOR ONLINE READING ONLY
           Hatua za ufundishaji
             (i)   Waongoze wanafunzi kubungua bongo kwa kufanya shughuli
                  ya 2.19 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
                  chagua wanafunzi wachache wajibu maswali utakayowauliza.
                  Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kwa kujibu au kuuliza
                  maswali  yanayochochea  mjadala.  Rekebisha  upungufu
                  unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.

           Majibu

           Majibu  ya  shughuli  ya  2.19  yatatokana  na  uelewa  wa  mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi akusanye methali tano (5) zinazoonya
           kuhusu  utovu wa nidhamu na misemo mitano (5) inayohamasisiha
           ushirikiano katika maisha. Pia, mwanafunzi aeleze umuhimu wa semi
           hizo katika maendeleo ya jamii.

           Shughuli ya 2.20

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili shughuli
                  ya 2.20 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha
                  kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu katika majadiliano.

             (ii)  Waelekeze  wanafunzi kufanya uwasilishaji kwa kuwauliza
                  maswali na wanafunzi wajibu kuhusu mchango wa fasihi
                  katika maendeleo ya jamii. Rekebisha upungufu unaojitokeza
                  ili kuleta uelewa wa pamoja.







             18                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   18
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   18    23/06/2024   17:48
   19   20   21   22   23   24   25   26   27   28   29