Page 27 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 27
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Mahitaji: Chati/mti wenye vipengele vya fani na maudhui
yaliyorekodiwa na matini na makala za kifasihi, magazeti,
maigizo, mashairi na tamthiliya zilizorekodiwa, kamusi,
vitabu teule, chati ya alama za LAT
FOR ONLINE READING ONLY
Somo la 1: Mtazamo kuhusu fani na maudhui
Shughuli ya 3.1
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika jozi, wakitafakari mitazamo
kuhusu fani na maudhui.
(ii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha darasani mawazo yao
kuhusiana na mitazamo hiyo kwa njia ya kushindanisha jozi.
(iii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi ili kujadili shughuli
ya 3.1 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki kikamilifu.
(iv) Waongoze wanafunzi kufanya uwasilishaji. Chagua baadhi ya
vikundi kuwasilisha kwa niaba ya vingine. Zingatia ushiriki
wa kila kikundi wakati wa uwasilishaji wa kazi za vikundi.
Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji ili
kuwa na uelewa wa pamoja.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 3.1 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
shughuli hii, mwanafunzi ajikite katika mitazamo miwili yaani kidhanifu
na kiyakinifu. Katika mtazamo wa kidhanifu mwanafunzi aeleze namna
vipengele vya fani na maudhui vinavyoweza kutenganishwa. Pia,
mtazamo wa kiyakinifu mwanafunzi aeleze namna vipengele vya fani
na maudhui haviwezi kutenganishwa.
Kiongozi cha Mwalimu 21
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 21 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 21