Page 23 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 23

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


             (iii)  Waongoze  wanafunzi  kurekebisha  upungufu unaojitokeza
                  katika mdahalo huo ili kuleta uelewa wa pamoja.

           Majibu

           FOR ONLINE READING ONLY
           Majibu  ya  shughuli  ya  2.17  yatatokana  na  uelewa  wa  mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi  aeleze  kwa mifano namna fasihi
           simulizi ilivyochangia kupatikana kwa fasihi andishi.



             Somo la 4:  Athari za sayansi na teknolojia katika maendeleo ya
                        fasihi simulizi na fasihi andishi

           Shughuli ya 2.18

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kuangalia au kusikiliza vipindi
                  mbalimbali vinavyohusiana na fasihi simulizi vilivyorekodiwa
                  au vinavyorushwa, kisha wakae katika jozi ili kufanya shughuli
                  ya 2.18 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waelekeze wanafunzi kuandaa kazimradi inayohusu athari za
                  sayansi na teknolojia katika maendeleo ya fasihi simulizi na
                  fasihi andishi. Katika majadiliano, sisitiza matumizi ya mifano
                  ili kuthibitisha hoja zinazotolewa. Hakikisha kila mwanafunzi
                  anashiriki  kikamilifu  na kuchukua  nukuu. Hakikisha
                  unahitimisha majadiliano hayo.

           Majibu
           Majibu ya shughuli ya 2.18 na yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze athari zinazotokana na vipindi
           hivyo kurushwa na vyombo mbalimbali vya habari.









                 Kiongozi cha Mwalimu                                    17
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   17    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   17
   18   19   20   21   22   23   24   25   26   27   28