Page 18 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 18
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Majibu
Majibu ya shughuli ya 2.8 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atumie mifano kubainisha sifa za
fasihi andishi na tanzu zake.
FOR ONLINE READING ONLY
Shughuli ya 2.9
Hatua za ufundishaji
(i) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi kisha kutumia
vyanzo vya mtandaoni au maktabani kufanya shughuli ya
2.9 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki kikamilifu.
(ii) Waongoze wanafunzi kufanya uwasilishaji. Chagua wanafunzi
wachache kuwasilisha kazi waliyoijadili katika vikundi vyao.
Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 2.9 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze kwa mifano dhana na
chimbuko la ushairi wa Kiswahili.
(iii) Mwongoze mwanafunzi kufanya zoezi la 2.2 lililomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi. Sahihisha na toa mrejesho wa kazi
waliyoifanya.
Majibu
Majibu ya zoezi la 2.2 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi katika
kuhusiana na maswali husika. Mwanafunzi ashadadie hoja zake kwa
mifano dhahiri.
12 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 12 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 12