Page 13 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 13

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Mahitaji: Chati/ mti wenye tanzu za fasihi simulizi na fasihi andi-
                     shi, ramani ya dhana, nyimbo, mashairi, na maigizo ya-
                     liyorekodiwa, matini na makala za magazetini, kamusi,
                     chati ya alama za LAT
           FOR ONLINE READING ONLY


             Somo la 1: Tanzu na vipera vya fasihi simulizi na fasihi andishi


           Shughuli ya 2.1

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi  kubungua bongo kuhusu matumizi  ya
                  fasihi kama nyenzo ya kuwasilisha mawazo katika miktadha
                  mbalimbali  kisha tumia  kibaofumbo  ili  kupata  baadhi  ya
                  wanafunzi  kujibu maswali  hayo. Rekebisha  upungufu
                  unaojitokeza.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo vya mtandaoni au
                  maktabani  kusoma matini kuhusu shughuli ya 2.1 iliyomo
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (iii)  Waelekeze wanafunzi kukaa katika jozi au vikundi ili kujadili
                  shughuli ya 2.1 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
                  kuwasilisha wawasilishe kazi zao walizojadili katika vikundi
                  kwa ajili ya majadiliano zaidi.

             (iv)  Rekebisha upungufu unaojitokeza  wakati wa uwasilishaji ili
                  kuleta uelewa wa pamoja.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 2.1 yatatokana  na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze kwa mifano kuhusu dhana ya
           tanzu na vipera kwa kuongozwa na maswali yaliyopo katika Kitabu
           cha Mwanafunzi. Majibu ya shughuli hii yanaweza kueleza tofauti kwa
           kuzingatia vigezo vya utunzi, uwasilishaji na uhifadhi.


                 Kiongozi cha Mwalimu                                     7
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   7     23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   7
   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18