Page 9 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 9
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
zaidi. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki katika uwasilishaji
kwa kutoa mawazo yake na au kuuliza maswali.
(ii) Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji
FOR ONLINE READING ONLY
darasani kuhusu mitazamo ya dhana za fasihi.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 1.3 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze mitazamo ya dhana ya fasihi
kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali.
Shughuli ya 1.4
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili shughuli
ya 1.4 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha chagua
baadhi vikundi vitakavyowasilisha hoja hizo kwa niaba ya
vikundi vingine. Kumbuka kuchanganya vikundi hivyo ili
wanafunzi wapeane maarifa mbalimbali. Rekebisha upungufu
unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.
(ii) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 1.1 lililomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi kisha kusanya kazi za wanafunzi,
sahihisha na kutoa mrejesho.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 1.4 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze ubora na upungufu wa kila
mtazamo wa dhana ya fasihi kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali.
Majibu ya zoezi lililomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi yatatokana
na uelewa wa mwanafunzi na maswali husika.
Kiongozi cha Mwalimu 3
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 3 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 3