Page 7 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 7

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari





               Sura ya

               Kwanza              Dhana na chimbuko la fasihi
           FOR ONLINE READING ONLY





                         Utangulizi
            Katika  sura hii, mwanafunzi atajifunza  juu ya dhana ya fasihi,
            mitazamo mbalimbali ya dhana ya fasihi, na ubora na udhaifu wa
            mitazamo hiyo. Vilevile, atajifunza juu ya nadharia za chimbuko la
            fasihi. Baada ya kujifunza vipengele hivyo, ataweza kukuza uelewa
            na kutathmini masuala  ya kifasihi kwa jumla. Mwalimu utapata
            baadhi ya mbinu zitakazokuwezesha katika ujenzi wa umahiri huu
            kwa mwanafunzi.




           •                 Shughuli za kutendwa na mwanafunzi


           (a)  Kufafanua dhana ya fasihi

           (b)  Kujadili nadharia za chimbuko la fasihi

           Mahitaji:  Mchoro wa sanaa na matawi yake, matini za kifasihi, kamusi,
                     chati ya alama za LAT


             Somo la 1: Dhana ya fasihi


           Shughuli ya 1.1 na 1.2

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufikiri juu ya umuhimu wa fasihi katika
                  maisha  ya  kila  siku  kwenye  kipengele  cha  fikiri  kilichomo

                 Kiongozi cha Mwalimu                                     1
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   1     23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   1
   2   3   4   5   6   7   8   9   10   11   12