Page 10 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 10
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Somo la 2: Nadharia za chimbuko la fasihi
Shughuli ya 1.5
FOR ONLINE READING ONLY
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kusoma matini mbalimbali zinazopatikana
mkondoni au maktabani zinazohusiana na shughuli ya 1.5
iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki katika kupakua na kuchambua matini
hizo.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi ili kuchambua
matini za nadharia za chimbuko la fasihi. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki katika majadiliano.
(iii) Waongoze wanafunzi kufanya uwasilishaji, chagua vikundi
vichache kuwasilisha nadharia za chimbuko la fasihi
walizozichambua kwa niaba ya wengine. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki kwa kutoa mawazo na kuuliza maswali
wakati wa uwasilishaji. Rekebisha upungufu unaojitokeza.
(iv) Hitimisha kwa kutoa maelezo yanayohusiana na shughuli
husika.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 1.5 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
shughuli hii, mwanafunzi aeleze kwa mifano nadharia za chimbuko la
fasihi kwa kutumia vyanzo mbalimbali atakavyokuwa amevisoma au
kujadili darasani.
Shughuli ya 1.6
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi ili kujadili shughuli
ya 1.6 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha kila
4 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 4
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 4 23/06/2024 17:48