Page 15 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 15
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
kila mwanafunzi anashiriki na kuchukua dondoo za hoja
zinazojadiliwa. Rekebisha dosari zinazojitokeza katika
majadiliano.
(iii) Waongoze wanafunzi kufanya uwasilishaji. Chagua wanafunzi
FOR ONLINE READING ONLY
wachache kuwasilisha hoja zao. Hakikisha kila mwanafunzi
anashiriki kikamilifu. Rekebisha dosari zinazojitokeza katika
uwasilishaji.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 2.3 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi afafanue kwa mifano semi na vipera
vyake kama vile methali, misemo, mizungu na vitendawili. Ufafanuzi
huo uzingatie umuhimu wa kila kipera katika jamii.
Shughuli ya 2.4
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika jozi ili kutumia maktaba au
maktaba mtandao na vyanzo vingine kusoma matini zinazohusu
shughuli ya 2.4 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu kupakua na
kuchambua matini hizo huku akichukua dondoo muhimu.
(ii) Waelekeze wanafunzi kuandaa na kutunga mjadala unaohusu
ushairi simulizi wa Kiswahili na vipera vyake. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki kikamilifu kwa kuchangia hoja katika
mjadala huo.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 2.4 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi afafanue kwa mifano maana, sifa na
vipera vya ushairi simulizi. Mwanafunzi aeleze namna ushairi simulizi
unavyotofautiana na ushairi andishi.
Kiongozi cha Mwalimu 9
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 9 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 9