Page 16 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 16

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Shughuli ya 2.5

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya kazi binafsi kutokana na
           FOR ONLINE READING ONLY
                   shughuli ya 2.5 (a) na (b) zilizomo  kwenye Kitabu cha
                   Mwanafunzi, kisha kukusanya kwa ajili  ya kusahihisha na
                   kutoa maboresho ya kazi ya kila mwanafunzi.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 2.5 (a) na (b) yatatokana  na uelewa wa
           mwanafunzi.  Mwanafunzi azingatie  hatua  na kanuni za utunzi
           kulingana na kipera atakachokichagua. Pia, katika utunzi wa jigambo
           mwanafunzi  azingatie  kanuni za utunzi  wa majigambo na kuweka
           ushikamani wa mada husika.

           Shughuli ya 2.6

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze  wanafunzi  kukaa  katika  vikundi  na  kujadili
                   shughuli  ya  2.6 iliyomo  kwenye  Kitabu  cha  Mwanafunzi,
                   kisha wawasilishe darasani. Hakikisha kila mwanafunzi
                   anashiriki kikamilifu  katika uwasilishaji na rekebisha
                   upungufu unaojitokeza.

             (ii)  Hitimisha shughuli kwa kutoa mrejesho wa shughuli hiyo.

           Majibu

           Majibu  ya  shughuli  ya  2.6  yatatokana  na  uelewa  wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi afafanue kwa mifano maana, sifa na
           aina za sanaa za maonesho. Mwanafunzi aeleze kwa ubayana namna
           sanaa  za  maonesho  zinavyoweza  kutofautiana  na  kazi  zingine  za
           kifasihi au kisanaa.





             10                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   10
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   10    23/06/2024   17:48
   11   12   13   14   15   16   17   18   19   20   21