Page 19 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 19
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Shughuli ya 2.10
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo vya mtandoni na
maktabani katika jozi au vikundi ili kufanya shughuli ya 2.10
FOR ONLINE READING ONLY
iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi kisha wawasilishe
darasani kwa majadiliano zaidi. Hakikisha kila mwanafunzi
anashiriki katika uwasilishaji. Rekebisha upungufu unaojitokeza
ili kuleta uelewa wa pamoja.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 2.10 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze dhana na historia ya hadithi
fupi ya Kiswahili.
Shughuli ya 2.11
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo mbalimbali kufanya
shughuli binafsi ya 2.11 iliyomo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi. Kila mwanafunzi ashiriki kufanya kazi binafsi.
(ii) Unaweza kuwaelekeza wanafunzi kutumia njia ya changanya-
kete ili kuchagua wanafunzi wachache kuwasilisha hadithi
zao walizosoma na kuzichambua. Hakikisha kila mwanafunzi
anashiriki kwa kuchangia mawazo yake na kuwauliza maswali
ili kuchochea majadiliano.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 2.11 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi abainishe aina za hadithi fupi na
kuchambua maudhui yaliyomo katika hadithi hizo.
Kiongozi cha Mwalimu 13
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 13 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 13