Page 21 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 21
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha wawasilishe
darasani. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu.
Sahihisha makosa yanayojitokeza wakati wa uwasilishaji.
Majibu
FOR ONLINE READING ONLY
Majibu ya shughuli ya 2.14 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi afafanue dhana na aina za riwaya.
Shughuli ya 2.15
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika jozi na kufanya shughuli
ya 2.15 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha
kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu kutoa mawazo yake
kuhusiana na shughuli husika na kuchukua nukuu. Kusanya
kazi zao, sahihisha na rekebisha dosari zinazojitokeza kwa
kutoa mrejesho kwa wakati.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 2.15 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi aeleze kwa mifano tofauti zilizopo
kati ya riwaya na hadithi fupi.
(i) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi vya wanafunzi
wasiopungua watano watano (5) kisha kufanya zoezi la 2.3
lililomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, sahihisha na kutoa
mrejesho wa zoezi hilo.
Majibu
Majibu ya zoezi la 2.3 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Mwanafunzi atumie mifano kushadidia hoja zake.
Kiongozi cha Mwalimu 15
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 15 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 15