Page 17 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 17

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Shughuli ya 2.7

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo mbalimbali kukusanya
           FOR ONLINE READING ONLY
                  michezo  mitatu  ya watoto katika shughuli ya 2.7 iliyomo
                  kwenye  Kitabu  cha  Mwanafunzi,  kisha  bainisha  mbinu  za
                  kisanaa zilizotumika katika utunzi wa michezo hiyo. Hakikisha
                  kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu huku akichukua nukuu.

             (ii)  Waongoze  wanafunzi  kukusanya  kazi  zao  ili  kurekebisha  na
                  kuondoa dosari zinazojitokeza,  kisha hitimisha  kwa kutoa
                  mrejesho wa shughuli hiyo.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 2.7 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
           shughuli hii, mwanafunzi abainishe mbinu mbalimbali  za kisanaa
           zilizotumika katika kutunga michezo aliyoichagua.

             (iii)  Waelekeze  wanafunzi kufanya zoezi la 2.1 lililomo kwenye
                  Kitabu cha Mwanafunzi.

           Majibu
           Majibu ya zoezi la 2.1 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi kuhusiana
           na maswali hayo. Mwanafunzi atumie mifano dhahiri kutetea hoja kwa
           kila swali.


           Shughuli ya 2.8
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo vya mtandaoni au
                  vinginevyo kufanya shughuli ya 2.8 iliyomo  kwenye Kitabu
                  cha Mwanafunzi, kisha kila mwanafunzi akusanye kazi yake
                  kwa ajili ya kusahihisha na kuondoa dosari zitakazojitokeza.




                 Kiongozi cha Mwalimu                                    11
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   11    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   11
   12   13   14   15   16   17   18   19   20   21   22