Page 12 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 12
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Sura ya
Pili Fasihi simulizi na fasihi andishi
Utangulizi
Katika sura hii, mwanafunzi atajifunza kuhusu tanzu na vipera vya
fasihi simulizi na fasihi andishi. Pia, atajifunza namna ya kuhusianisha
fasihi simulizi na fasihi andishi. Aidha, atajifunza kuhusu mchango
wa fasihi simulizi katika maendeleo ya fasihi andishi na mchango wa
fasihi simulizi na fasihi andishi katika maendeleo ya jamii. Baada ya
kujifunza, ataweza kuchambua na kutunga kazi za kifasihi kulingana
na tanzu na kipera husika. Mwalimu utapata baadhi ya mbinu
zitakazokuwezesha katika ujenzi wa umahiri huu kwa mwanafunzi.
FOR ONLINE READING ONLY
Shughuli za kutendwa na mwanafunzi
(a) Kufafanua tanzu na vipera vya fasihi simulizi na fasihi andishi
(b) Kujadili uhusiano wa fasihi simulizi na fasihi andishi
(c) Kueleza mchango wa fasihi simulizi katika maendeleo ya fasihi
andishi
(d) Kutathmini athari za sayansi na teknolojia katika maendeleo ya
fasihi simulizi na andishi
(e) Kujadili mchango wa fasihi simulizi na fasihi andishi katika
maendeleo ya jamii
(f) Kuhusianisha fasihi simulizi na fasihi andishi
6 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 6
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 6 23/06/2024 17:48