Page 14 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 14
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Shughuli ya 2.2
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo mbalimbali vya maarifa
FOR ONLINE READING ONLY
kusoma matini zinazohusu shughuli ya 2.2 iliyomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika jozi au vikundi ili kujadili
shughuli ya 2.2 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Katika majadiliano, kila mwanafunzi ashiriki kikamilifu kwa
kutoa mawazo juu ya alichokisoma katika matini.
(iii) Waongoze wanafunzi kufanya uwasilishaji. Chagua wanafunzi
wachache kuwasilisha kazi zao kwa niaba ya wengine.
Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kwa kuchangia mawazo
na au kuuliza maswali ili kuboresha kazi zilizowasilishwa.
Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji ili
kuleta uelewa wa pamoja.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 2.2 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
shughuli hii, mwanafunzi afafanue kwa mifano utanzu wa hadithi na
vipera vyake. Majibu yaeleze utanzu wa hadithi na uhusiano wa vipera
vyake kama vile ngano, vigano, tahiri, soga na visasili.
Shughuli ya 2.3
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo vya mtandaoni au
maktabani kusoma matini mbalimbali zinazohusu shughuli ya
2.3 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika jozi na kujadili shughuli
ya 2.3 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha
8 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 8
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 8 23/06/2024 17:48