Page 8 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 8

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha wakae katika jozi na
                  washirikishane yale waliyotafakari.

             (ii)  Wanafunzi wabungue bongo kuhusu dhana ya fasihi kulingana
                  na wataalamu mbalimbali ili kupata maarifa yao ya awali.
           FOR ONLINE READING ONLY
             (iii)  Waelekeze  wanafunzi kukaa katika  vikundi au jozi au njia
                  nyingine unayoona inafaa  kulingana  na mazingira  yako na
                  kujadili  shughuli ya 1.1 na 1.2 zilizomo  kwenye Kitabu
                  cha  Mwanafunzi.  Hakikisha  kila  mwanafunzi  anashiriki
                  katika  mjadala.  Rekebisha  dosari zinazojitokeza  wakati  wa
                  majadiliano.

             (iv)  Waelekeze wanafunzi kuandaa uwasilishaji. Chagua wanafunzi
                  wachache kuwakilisha wengine. Katika uwasilishaji, hakikisha
                  kila  mwanafunzi  anashiriki  kwa kutoa  mawazo  yake  au
                  kuuliza maswali. Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa
                  uwasilishaji.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 1.1 na 1.2 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika  shughuli ya 1.1, mwanafunzi  abainishe  matini  za kifasihi
           kulingana  na ufahamu  na uzoefu  wake. Katika  shughuli ya 1.2
           mwanafunzi atoe maoni kuhusu dhana ya fasihi kwa mujibu wa ufahamu
           wake na vyanzo alivyovirejelea.


           Shughuli ya 1.3

           Hatua za ufundishaji

              (i)  Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi na kuchambua matini
                  mbalimbali zinazohusiana na shughuli ya 1.3 iliyomo kwenye
                  Kitabu cha Mwanafunzi. Kisha, toa nafasi ya kila kikundi

                  kuwasilisha mitazamo hiyo darasani kwa ajili ya majadiliano




              2                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   2
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   2     23/06/2024   17:48
   3   4   5   6   7   8   9   10   11   12   13