Page 28 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 28

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari



             Somo la 2: Uhusiano wa fani na maudhui katika kazi za fasihi


           Shughuli ya 3.2(a)
           FOR ONLINE READING ONLY
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kusoma hadithi teule mojawapo, kisha
                  wakae katika jozi wajadili shughuli ya 3.2(a) iliyomo kwenye
                  Kitabu cha Mwanafunzi, hakikisha kila mwanafunzi anashiriki
                  kikamilifu huku akiandika tini.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kuhitimisha kwa kutoa maelezo ya jumla
                  yanayohusiana na shughuli husika.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 3.2 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi  achambue  vipengele  vya fani na
           maudhui katika hadithi teule atakayoichagua  kwa kuongozwa na
           maswali (i) - (iv). Pia mwanafunzi aoneshe uhusiano wa fani na maudhui
           katika kazi yoyote ya fasihi.


           Shughuli ya 3.2 (b)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kusikiliza au kusoma kazi yoyote ya fasihi
                  kisha kukaa katika jozi ili kuchambua uhusiano wa vipengele
                  vya fani na maudhui katika kazi hiyo.

             (ii)  Waelekeze  wanafunzi kubadilishana  kazi zao na kila jozi
                  isome kazi ya wenzao kisha kukosoa dosari watakazozibaini na
                  kurudisha tena kwa wahusika.

             (iii)  Waongoze  wanafunzi  kuuliza  maswali  yatakayochochea
                  mjadala na kila mwanafunzi ashiriki kujibu maswali. Rekebisha
                  upungufu unaojitokeza


             22                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   22
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   22    23/06/2024   17:48
   23   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33