Page 57 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 57
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.16 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli 4.16 (a), mwanafunzi atachambua athari za kiimani na
FOR ONLINE READING ONLY
mitazamo katika nyimbo kwa kujibu maswali yaliyotolewa.
Shughuli ya 4.16(b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kusoma na kuchambua mashairi mawili
kutoka katika diwani teule, kisha kukaa katika jozi na kujadili
shughuli ya 4.16 (b) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kufanya uwasilishaji, chagua wanafunzi
wachache kuwasilisha kazi zao darasani kwa majadiliano zaidi
huku ukirekebisha upungufu unaojitokeza.
(iii) Hitimisha kwa kutoa maelezo ya jumla kuhusiana na shughuli
husika.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.16 (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli 4.16 (b), mwanafunzi atachambua athari za kiimani na
mitazamo katika mashairi mawili kutoka kwenye diwani teule.
Shughuli ya 4.17(a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi na kusoma matini
fupi ya tamthiliya iliyomo katika shughuli ya 4.17 (a) katika
Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha kazi zao darasani kwa
majadiliano zaidi huku ukirekebisha upungufu unaojitokeza
Kiongozi cha Mwalimu 51
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 51 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 51