Page 60 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 60
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
(f) Kutathmini kazi za fasihi kwa kutumia misingi ya ujenzi wa
hoja zenye mantiki na ushawishi; na
(g) Kuwasilisha hoja zenye mantiki na ushawishi kwa kutumia
maarifa ya kifasihi.
FOR ONLINE READING ONLY
Mahitaji
Matini na makala za kifasihi, magazeti, hadithi, nyimbo, mashairi na
maigizo yaliyorekodiwa, vitabu teule, kamusi na vinginevyo.
Somo la 1: Vigezo vya ujenzi wa ujumi katika kazi za fasihi
Shughuli ya 5.1
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kusikiliza au kutazama video za nyimbo
tano (5) ambazo anadhani ni nzuri na zingine tano (5) ambazo
anadhani ni mbaya kama inavyoelekezwa katika shughuli ya
5.1 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waongoze wanafunzi kuchambua maudhui ya nyimbo hizo
kisha kueleza sababu za nyimbo hizo kuwa au nzuri au mbaya.
Ongoza mjadala kisha rekebisha upungufu unaojitokeza.
Majibu
Majibu ya shughuli 5.1 yatategemeana na uelewa wa mwanafunzi.
Mwanafunzi ajibu kulingana nyimbo atakazozichagua.
Shughuli ya 5.2 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi kujadili shughuli
ya 5.2 (a) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha
54 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 54
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 54 23/06/2024 17:48