Page 56 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 56
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Shughuli ya 4.15(b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika jozi au vinginevyo
FOR ONLINE READING ONLY
kujadiliana shughuli ya 4.15(b) iliyomo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kufanya uwasilishaji kisha, chagua
wanafunzi wachache kuwasilisha kazi zao darasani kwa
majadiliano zaidi huku ukirekebisha upungufu unaojitokeza.
(iii) Hitimisha kwa kutoa maelezo ya jumla kuhusu shughuli husika.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.15(b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua athari za kiimani na
mitazamo katika nyimbo mbili za bongo fleva atakazozichambua.
Shughuli ya 4.16(a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo vya mtandaoni au
vinginevyo kupakua na kusikiliza nyimbo mbalimbali za bongo
fleva, kisha kufanya kazi binafsi ya shughuli ya 4.16 (a) iliyomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Unaweza kuchagua wanafunzi wachache kuwasilisha kazi zao
au vinginevyo, hakikisha ushiriki wa kila mwanafunzi wakati
wa uwasilishaji. Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa
uwasilishaji
(iii) Hitimisha kwa kutoa maelezo ya jumla kuhusiana na shughuli
husika.
50 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 50
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 50 23/06/2024 17:48