Page 61 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 61
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
kila mwanafunzi anatoa mawazo yake wakati wa majadiliano.
Rekebisha dosari zinazojitokeza.
(ii) Waongoze wanafunzi kuandaa uwasilishaji wa uchambuzi
wa maudhui, kisha chagua baadhi ya vikundi ili kuwakilisha
FOR ONLINE READING ONLY
wenzao. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kwa kutoa
mchango au kuuliza maswali ili kuchochea majadiliano.
Sahihisha upungufu unaojitokeza katika uwasilishaji, kisha toa
mrejesho wa shughuli husika.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 5.2 (a) yatategemea uelewa wa mwanafunzi.
Mwanafunzi anapojibu, ajikite katika kutumia misingi ya ujenzi wa
ujumi aliyosoma darasani ili kuchambua shairi hilo.
Shughuli ya 5.2 (b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kusoma au kughani shairi lililomo katika
shughuli ya 5.2 (b) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waongoze wanafunzi kuchambua shairi hilo kwa kutumia
misingi ya ujumi. Ongoza mjadala huku ukirebisha upungufu
unaojitokeza.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 5. 2 (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua shairi kwa kuzingatia
misingi ya ujumi wakati kuhakiki shairi hilo.
Shughuli ya 5.2 (c)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kusoma diwani teule kama
inavyoelekezwa katika shughuli ya 5.2 (c) iliyomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi.
Kiongozi cha Mwalimu 55
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 55 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 55