Page 63 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 63
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Majibu
Majibu ya shughuli 5.3(a) yatategemeana na uelewa wa mwanafunzi.
Mwanafunzi ajibu maswali baada ya kusoma na kuchambua jigambo
hilo kwa kuongozwa na maswali yaliyotolewa.
FOR ONLINE READING ONLY
Shughuli ya 5.3(b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.3(b) iliyomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kutumia kifaa chochote cha TEHAMA
kupakua jigambo lolote, kisha kuchambua mbinu ambazo
mtunzi amezitumia kujenga ujumi katika jigambo hilo.
(iii) Sahihisha kazi ya kila mwanafunzi ili kuondoa dosari
zitakazojitokeza na toa mrejesho kwa wanafunzi wote.
Majibu
Majibu ya shughuli 5.3(b) yanaweza kutegemeana na uelewa wa
mwanafunzi. Majibu ya shughuli hii yajikite katika kuchambua mbinu
za kiujumi zilizotumika katika jigambo atakalochambua.
Shughuli ya 5.4(a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.4 (a) iliyomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika jozi ili kusoma matini fupi
ya tamthiliya, kisha kujibu maswali. Hakikisha kila mwanafunzi
anashiriki kikamilifu katika majadiliano. Sikiliza mjadala na
uliza maswali ili kupima ushiriki wa kila mwanafunzi.
Kiongozi cha Mwalimu 57
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 57 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 57