Page 67 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 67
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Shughuli ya 5.7 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.7 (a) iliyomo
FOR ONLINE READING ONLY
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi vya watu wasiozidi
wanne kujadili shughuli ya 5.7 (a) iliyomo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi. Kisha, wajibu maswali yanayotokana na matini
fupi ya tamthiliya ili kupata maana mbalimbali. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki. Rekebisha dosari pale zitapojitokeza.
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha uchambuzi wa mashairi
teule, kisha chagua vikundi vichache kuwasilisha kwa niaba
ya vingine. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kwa kutoa
mchango au kuuliza maswali. Sahihisha upungufu unaojitokeza.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 5.7 (a) yatategemea uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua maana mbalimbali kutoka
katika kipande cha tamthiliya.
Shughuli ya 5.7(b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kuchambua tamthiliya mbili teule.
Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu katika
uchambuzi na kuandika tini.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukusanya na kusahihisha kazi za
wanafunzi ili kuondoa upungufu unaojitokeza.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 5.7 (b) yatategemea uelewa wa mwanafunzi
na tamthiliya teule atakayoichambua. Katika kuchambua maana,
mwanafunzi atumie mifano kutoka katika tamthiliya husika.
Kiongozi cha Mwalimu 61
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 61 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 61