Page 69 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 69
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
(ii) Waelekeze wanafunzi kukusanya na kusahihisha kazi za
wanafunzi ili kuondoa upungufu unaojitokeza.
Majibu
FOR ONLINE READING ONLY
Majibu ya shughuli ya 5.8 (b) yatategemea uelewa wa mwanafunzi na
shairi atakalolichambua kutoka katika diwani teule. Katika uchambuzi,
mwanafunzi aoneshe namna mbinu za kifasihi zinavyochangia au
kutatiza kupatikana kwa maana kwa kutumia mifano kutoka katika
shairi husika.
Shughuli ya 5.9
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.9 iliyomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili shughuli
ya 5.9 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Hakikisha
kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu. Rekebisha dosari
zinazojitokeza.
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha, chagua vikundi vichache
kuwasilisha kazi yao kwa niaba ya wengine. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki kwa kutoa mchango au kuuliza maswali
ili kuendeleza mjadala. Sahihisha upungufu unaojitokeza katika
uwasilishaji, kisha toa mrejesho wa shughuli husika.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 5.9 yatategemea uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua namna mbinu za kifasihi
zinavyoathiri maana mbalimbali kutoka katika kipande cha tamthiliya.
Kiongozi cha Mwalimu 63
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 63 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 63