Page 73 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 73

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


             (ii)  Waelekeze  wanafunzi  kukusanya  na  kusahihisha  kazi  za
                  wanafunzi ili kuondoa upungufu unaojitokeza.

           Majibu

           FOR ONLINE READING ONLY
           Majibu ya shughuli ya 5.12 (b) yatategemea uelewa wa mwanafunzi
           kwa kuzingatia nafasi ya kazi ambayo mwanafunzi ataichagua. Katika
           uchambuzi, mwanafunzi aoneshe namna atakavyowasilisha hoja zenye
           mantiki na ushawishi katika kuigiza usaili wa nafasi ya kazi husika.

           Shughuli ya 5.12 (c)
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kutumia maarifa ya kifasihi kuwasilisha
                  hoja zenye mantiki na ushawishi wakati wa kuigiza kama
                  mgombea wa nafasi ya uongozi katika uchaguzi wa shuleni.
                  Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki  kikamilifu katika
                  kuandaa usaili wa kazi atakayoichagua na kuchukua nukuu.

             (ii)  Waelekeze  wanafunzi  kukusanya  na  kusahihisha  kazi  za
                  wanafunzi ili kuondoa upungufu unaojitokeza.

           Majibu
           Majibu ya shughuli ya 5.12 (c) yatategemea uelewa wa mwanafunzi
           kwa kuzingatia nafasi ya kazi ambayo mwanafunzi ataichagua. Katika
           uchambuzi, mwanafunzi aoneshe namna atakavyowasilisha hoja zenye
           mantiki na ushawishi katika kuigiza usaili wa nafasi ya uongozi.


             Somo la 6:  Maarifa ya kifasihi kuwasilisha hoja zenye mantiki
                        na ushawishi katika malumbano ya hoja


           Shughuli ya 5.13
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.13 iliyomo kwenye
                  Kitabu cha Mwanafunzi.


                 Kiongozi cha Mwalimu                                    67
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   67    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   67
   68   69   70   71   72   73   74   75   76   77   78