Page 76 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 76
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Sura ya
Sita Kubuni kazi changamani za fasihi
FOR ONLINE READING ONLY
Utangulizi
Katika sura hii, mwanafunzi atajifunza kuhusu miktadha inayochochea
utunzi wa kazi changamani za fasihi; fursa zinazohusiana na utunzi
na uchapishaji wa kazi za fasihi; na mchango wa TEHAMA katika
kuongeza fursa zinazotokana na kazi za fasihi. Pia, atajifunza hatua,
kanuni za utunzi, na kutunga kazi za fasihi simulizi na fasihi andishi.
Umahiri utakaomjengea mwanafunzi utamwezesha kutunga maigizo,
mashairi na hadithi za watoto na kuzitumia kazi hizo kama fursa
ya kujiingizia kipato binafsi na jamii kwa ujumla. Mwalimu utapata
mbinu na utaratibu utakaokuwezesha katika ujenzi wa umahiri huu
kwa mwanafunzi.
Shughuli za kutendwa na mwanafunzi
(a) Kueleza miktadha inayochagiza utunzi wa kazi za fasihi.
(b) Kufafanua fursa mbalimbali zinazotokana na kazi za kifasihi
za Kiswahili.
(c) Kueleza mchango wa TEHAMA katika kutambua fursa
zinazotokana na kazi za fasihi.
(d) Kufafanua hatua za utunzi wa kazi za kifasihi.
(e) Kuchambua kanuni za utunzi na kutunga maigizo.
70 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 70
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 70 23/06/2024 17:48