Page 79 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 79

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Majibu
           Majibu ya shughuli ya 6.2 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
           shughuli hii, mwanafunzi aeleze  kwa mifano fursa zinazochochea
           utunzi wa kazi za kifasihi.
           FOR ONLINE READING ONLY


             Somo la 3:  Mchango wa  TEHAMA katika kutambua  fursa
                        zinazotokana na kazi za kifasihi

           Shughuli ya 6.3

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Wauulize  wanafunzi  maswali  kuhusu dhana  ya TEHAMA,
                  majukwaa ya kidijiti,  na jinsi ya kutumia majukwaa hayo.
                  Wanafunzi  wajibu  maswali  hayo  kutokana  na  uelewa wao.
                  Rekebisha majibu  yao kwa kuelekeza  namna ya kutumia
                  majukwaa hayo.

             (ii)  Waelekeze wanafunzi kupakua, kusoma na kueleza mchango
                  wa  TEHAMA katika  kutambua  fursa zinazotokana na  kazi
                  za kifasihi kama shughuli ya 6.3 iliyomo kwenye Kitabu cha
                  Mwanafunzi.

             (iii)  Waongoze wanafunzi kuandaa malumbano ya hoja kuhusu
                  mchango wa TEHAMA katika kutambua fursa zinazotokana na
                  kazi za kifasihi, kisha hamasisha kila mwanafunzi kushiriki.

             (iv)  Waelekeze wanafunzi kuandaa uwasilishaji ambao utachagiza
                  kila  mwanafunzi  kushiriki  kwa  kutoa  mchango  na  kuuliza
                  maswali ili kulifanya darasa kuwa changamshi, huku
                  ukiwasahihisha na kuondoa dosari zinazojitokeza.
           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 6.3 yatatokana  na uelewa wa mwanafunzi.
           Majibu  yanaweza  hatua  za  kuandaa  na  kuchapisha kazi  za  kifasihi


                 Kiongozi cha Mwalimu                                    73
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   73    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   73
   74   75   76   77   78   79   80   81   82   83   84