Page 83 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 83

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Majibu
           Majibu ya shughuli 6.7 (a) yatatokana na mawazo wa mwanafunzi. Pia,
           yanaweza kuwa yale yaliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

           FOR ONLINE READING ONLY
           Shughuli ya 6.7 (b)
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 6.7 (b) iliyomo
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waelekeze  wanafunzi  kupakua  igizo  lolote  kwa kutumia
                  kifaa  cha  TEHAMA kinachopatikana  katika  mazingira  ya
                  shuleni,  kisha kuchambua  kanuni zilizotumika  katika utunzi
                  wa igizo hilo. Au waagize mwanafunzi kupakua na kutazama
                  au kusikiliza igizo lolote akiwa nyumbani, kisha wachambue
                  kanuni zilizotumika katika utunzi wa igizo husika.

             (iii)  Waongoze wanafunzi kuandaa uwasilishaji wa kanuni za utunzi
                  wa maigizo.  Chagua  wanafunzi  wachache  wawasilishe  na
                  wengine wasikilize, huku wakichangia mawazo yao na kuuliza
                  maswali  kuhusu kile  kinachowasilishwa.  Rekebisha  dosari
                  zinazojitokeza.
           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 6.7 (b) yatatokana na mawazo ya mwanafunzi.
           Pia, yanaweza kuwa yale yaliyopo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
           Katika  kufanya  shughuli hii,  mwanafunzi  abainishe  wazi  tofauti
           zilizomo katika vipengele vya matumizi ya dayalojia, uumbaji wa visa
           na vitendo, ujitokezaji wa migogoro, uumbaji wa wahusika, uchaguzi
           wa mandhari na namna mtunzi anavyogusa hisia za hadhira katika
           utunzi wa maigizo vinavyotofautiana na katika ushairi na hadithi za
           watoto.







                 Kiongozi cha Mwalimu                                    77
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   77    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   77
   78   79   80   81   82   83   84   85   86   87   88