Page 85 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 85
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Majibu
Majibu ya shughuli ya 6.9 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Pia, yanaweza kuwa yale yaliyopo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Mwanafunzi aeleze namna anavyotumia lugha ya kishairi, muundo,
FOR ONLINE READING ONLY
muwala, taswira na ishara, mtindo na utosherevu wa shairi kuanzia
kwenye mshororo/mstari, kwenye ubeti na shairi zima. Mambo haya
yabainishwe vizuri kishairi na namna yanavyotofautiana yanapotumika
katika tanzu zingine.
Shughuli ya 6.10 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kughani au kusoma mashairi mawili
kutoka katika diwani teule, kisha wachambue kanuni
zilizotumika katika utunzi wa mashairi. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki kikamilifu katika uchambuzi na
kuandika tini.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukusanya kazi, kisha sahihisha kazi za
wanafunzi ili kuondoa upungufu unaojitokeza.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 6.10 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi
na diwani teule atakazozichambua.
Shughuli ya 6.10 (b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 6.10(b) iliyomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Kusanya kazi na sahihisha kisha toa mrejesho.
Kiongozi cha Mwalimu 79
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 79 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 79