Page 86 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 86
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Somo la 7: Kanuni za utunzi wa kutunga hadithi za watoto
Shughuli ya 6.11 (a) na (b)
FOR ONLINE READING ONLY
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kueleza kuhusu dhana ya hadithi za
watoto.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukusanya vitabu vya hadithi mbalimbali
za watoto, kisha vigawe katika makundi kwa kufuata umri
na hatua za usomaji. Wagawe wanafunzi katika vikundi kwa
kufuata idadi ya makundi ya vitabu, wachambue sifa na kanuni
za utunzi wa hadithi zilizomo katika vitabu hivyo.
(iii) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi walivyounda kujadili
sifa na kanuni za hadithi za watoto. Hakikisha kila mwanafunzi
anashiriki katika kutoa mawazo yake. Tembelea kila kikundi ili
kurekebisha dosari zinazojitokeza katika majadiliano.
(iv) Waongoze wanafunzi kufanya uwasilishaji, kila kikundi
kichague mwakilishi awasilishe kazi yao na wanafunzi wengine
washiriki kwa kuchangia hoja na kuuliza maswali. Rekebisha
dosari zinazojitokeza katika uwasilishaji.
Majibu
Majibu ya shughuli 6.11(a) na (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Pia, yanaweza kuwa yale yaliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Mwanafunzi aeleze upekee wa utungaji wa hadithi za watoto
unavyotofautiana na utunzi wa hadithi za watu wazima.
80 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 80 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 80