Page 84 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 84
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Shughuli ya 6.8
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kubainisha masuala mtambuka kwa njia
FOR ONLINE READING ONLY
ya bungua bongo.
(ii) Wagawe wanafunzi katika vikundi, kisha watunge igizo fupi kwa
kufuata kanuni za utunzi. Kila kikundi kitachagua mada moja
na kuiumbia visa na matukio, kisha waoneshe walivyozingatia
kila hatua na kanuni za utunzi wa igizo hilo.
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha matini ya igizo kwa kuonesha
kila hatua na uzingativu wa kanuni za utunzi wa igizo lake.
Chagua vikundi vichache, viwasilishe huku wanafunzi wengine
wakisikiliza na kuchangia mawazo yao pamoja na kuuliza
maswali kuhusu kile kinachowasilishwa. Rekebisha dosari
zinazojitokeza.
Majibu
Majibu ya shughuli 6.8 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
utunzi, mwanafunzi azingatie hatua na kanuni za utunzi wa maigizo.
Somo la 6: Kanuni za utunzi na kutunga mashairi
Shughuli ya 6.9
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 6.9 iliyomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kusoma vyanzo mbalimbali kuhusu
kanuni zinazoongoza utunzi wa mashairi, kuuliza maswali,
kupima uelewa wa wanafunzi kuhusu kanuni za utunzi wa
mashairi na kueleza namna zinavyozitumika katika utunzi.
78 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 78
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 78 23/06/2024 17:48