Page 55 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 55
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Shughuli ya 4.14(b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi kujadiliana shughuli
ya 4.14(b) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
FOR ONLINE READING ONLY
wakusanye kazi zao. Sahihisha na toa mrejesho kwa wakati.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.14(b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua na kuhusianisha mitazamo
na matendo ya jamii kutoka kwenye tamthiliya teule mbili.
Somo la 5: Athari za kiimani na kimtazamo katika bongo fleva,
mashairi na tamthiliya zinavyojidhihirisha katika
jamii
Shughuli ya 4.15(a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo vya mkondoni na
vinginevyo kupakua na kusikiliza au kutazama nyimbo
mbalimbali zinazohamasisha mapambano ya maisha
zilizoimbwa na wasanii wa kike kisha kukaa katika vikundi
kufanya shughuli ya 4.15(a) iliyomo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi. Kila mwanafunzi afanye kazi binafsi kwa kujibu
maswali yaliyotolewa.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukusanya kazi walizozifanya katika
vikundi vyao, sahihisha na toa mrejesho.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.15(a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua athari za kiimani na
mitazamo katika wimbo huo kwa kujibu maswali yaliyotolewa.
Kiongozi cha Mwalimu 49
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 49 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 49