Page 15 - EDK_F5
P. 15

SURA YA KWANZA                                                   ELIMU KATIKA UISLAMU

        Malengo ya elimu katika mfumo wa kibepari


        Kwa vile kufanikiwa au kushindwa kwa mfumo wa ubepari kunatokana na sifa za
        wananchi wake, kwa hiyo lengo la msingi la elimu mbele ya watetezi wa ubepari
        ni kuwafanya raia kuwa wema kwa taifa. Hata hivyo, huyapa umuhimu usiofaa
        FOR ONLINE READING ONLY
        maendeleo  ya  mali  na  mafanikio  ya  kifedha.  Kuna  mapambano  ya  kuendelea

        miongoni mwa raia wake ili kuwatangulia wengine katika masuala ya utajiri. Pia
        katika  mfumo huu, maadili  hupoteza  thamani  yake, kwani hayana  thamani  ya
        kudumu. Wakati wowote kunapotokea mgongano wa maslahi kati ya serikali na
        maadili, wananchi hufundishwa kuacha maadili.


        Madhara ya mfumo wa elimu wa kibepari

        Kwa kuwa ubepari, huyapa umuhimu usiofaa maendeleo ya mali na mafanikio ya kifedha,
        kuna mapambano ya kuendelea miongoni mwa raia wake ili kuwatangulia wengine katika
        masuala ya utajiri. Kwa hiyo, utoaji wa elimu kupitia misingi ya kibepari, taasisi za elimu
        zinajikuta zinazalisha wahitimu wasio na maadili. Wahitimu wasiojali utu, uzalendo wa
        uadilifu katika kuhakikisha maslahi ya jamii kwa ujumla.

        Mfumo wa elimu katika Uislamu

        Kazi ya 1 2


        Shirikiana na wanafunzi wenzako kujadili maana na malengo ya elimu kwa mujibu
        wa Uislamu

        Uislamu ni mfumo kamili wa maisha, yaani haujaacha nyanja wala kipengele chochote
        cha maisha isipokuwa umekiweka bayana. Hii ndiyo dini pekee ya kweli na sahihi kwa
        wanadamu wote. Allah (S.W) amebainisha wazi kwamba mafanikio ya maisha haya na
        maisha ya akhera yanaweza kupatikana tu kwa kuikubali na kuifuata dini ya Uislamu.
        Kwa hiyo, mfumo wa elimu katika Uislamu umejengwa juu ya  misingi mikuu minane
        ifuatayo:

        Mosi,  Mungu mmoja,  Allah  (S.W) pekee  ndiye  Muumba, Mmiliki  na Mtawala  wa
        ulimwengu mzima. Wanadamu wote ni watumwa Wake na Yeye pekee ndiye anayestahiki
        kuwa Mfalme  na  Mwenye enzi.  Kila  mwanadamu  lazima  ahakikishe  anabaki  kuwa
        mtumwa Wake na kumuabudu Yeye pekee.

        Pili, Utume, Allah (S.W) aliwatuma Mitume wake kwa wanadamu kwa ajili ya uongofu
        wao. Mitume na Manabii, walileta amri zake kupitia vitabu mbalimbali. Mtume Muhammad
        (S.A.W) ndiye mjumbe wa mwisho wa Allah (S.W). Aliteremshiwa Qur’an ili aitumie

                                                   5
   10   11   12   13   14   15   16   17   18   19   20