Page 10 - EDK_F5
P. 10

DIBAJI


        Aidha, kuna vipengele  vipya ambavyo havikuwahi kufundishwa katika  Sekondari ya
        chini kama vile:

        (a)   Mchango wa Waislamu katikaTaaluma; katika sura ya kwanza;

        (b)   Vitimbi vya wapinzani dhidi ya Qur’an na athari zake; katika sura ya nne;
        FOR ONLINE READING ONLY
        (c)   Kufasiri Qur’an; katika sura ya tano;

        (d)   Hoja potofu zinazonasibishwa na Sunnah; katika sura ya sita; na

        (e)   Ahadi ya Utii; katika sura ya tisa.

        Kwa  ujumla, kitabu kinamuandaa mhitimu atakayemudu  kuamiliana  na jamii yenye
        imani, itikadi, maadili  na mitazamo  tofauti, atakayekuwa raia wa kimataifa,  msomi
        nyumbufu, mbunifu, msuluhishi na mtatuzi wa changamoto zinazomkabili mwanadamu
        na ulimwengu wake. Ingawa, tukiri kuwa kwa vile ni kitabu kilichoandikwa na wanadamu,
        hakikosi kuwa na dosari za hapa na pale, hivyo wasomaji wawe huru kuwasilisha maoni
        yao TISTA, kwa ajili ya marekebisho kwa matoleo yajayo.
                        Jumuiya ya Ufundishaji wa Masomo ya Kiislamu Tanzania (TISTA)












































                                                  viii
   5   6   7   8   9   10   11   12   13   14   15