Page 14 - EDK_F5
P. 14

SURA YA KWANZA                                                   ELIMU KATIKA UISLAMU


        Mfumo wa elimu wa ujamaa

        Ujamaa ni mfumo uliojikita katika ulimwengu wa kimaada au kupenda mali  na kupiga
        vita dini na maadili. Mfumo huu unapambana na matabaka kwa manufaa yake. Katika
        Ujamaa, watu na ubinafsi wao hauna thamani yoyote. Maisha ya raia na heshima yao iko
        FOR ONLINE READING ONLY
        chini ya serikali, ambayo pia inamiliki rasilimali zote za nchi.

        Lengo la elimu katika Ujamaa ni kuwawezesha wanadamu kuwa watumishi wasio na
        ubinafsi na wenye kujali maslahi ya jamii. Hufundishwa umuhimu wa kujenga uchumi
        wa pamoja badala ya uchumi binafsi. Pia, hujengwa kitabia kuchukia masuala ya dini na
        kupiga vita uwepo wa Allah (S.W).

        Madhara  ya mfumo wa elimu wa ujamaa


        Mfumo wa elimu wa kijamaa una madhara  yafuatayo:

        Kupinga uwepo wa Allah (S W), kunawafanya raia kutokuwa na uadilifu na kukosa
        maadili,  hutokea uharibifu wa maadili  katika  jamii.  Hujidhulumu  wenyewe na
        kuwadhulumu wengine. Wakati wowote wanapopata fursa hawafikirii mara mbili, iwe
        kuna madhara au hakuna.


        Utu wa mtu binafsi umeharibiwa, Mtu amepewa akili na vipawa vingine ili vimsaidie
        kuishi kwa uhuru na aweze kuwasaidia wengine, kwa kukosesha uhuru binafsi kinachotokea
        ni kuidumaza akili na vipawa vyake.

        Wanafunzi huwa katika vita  endelevu  dhidi ya tamaa, maoni  na  dhamira  zao.
        Wanakuwa na huzuni na msongo wa mawazo, kutokana na kutumikia nguvu za nje kwa

        lazima. Hakuna shaka kwamba wanafunzi kama hao hawawezi kamwe kuwa na utu au
        tabia za kimaadili.

        Uzalishaji mali umepewa nafasi ya kupitiliza, ujamaa  umewafanya  watu kama
        wanyama, kupitia mfumo wa elimu katika suala la uchumi, mtu anapaswa kuzalisha mali
        tu bila ya kuzingatia mambo ya kimaadili. Kwa hivyo, jambo muhimu kwao ni mtu kupata
        riziki na sio kitu kingine chochote.


        Watu wote wa taifa, isipokuwa wachache waliochaguliwa, wamegandishwa kisaikolojia.
        Watu wamenyimwa amani na utulivu wa dunia na maisha ya akhera. Hii ni kwa sababu
        saikolojia ya watu wa taifa la kijamaa inawaza kazi tu, akili haina muda wa kupumua au
        kufikiria mambo mengine, kama kutafakari kuhusu dunia na mustakabali na maisha ya
        akhera.


                                                   4
   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18   19