Page 13 - EDK_F5
P. 13

SURA YA KWANZA                                                   ELIMU KATIKA UISLAMU

        asiyetofautiana  na asiyesoma  katika  kutekeleza  majukumu  ya maisha,  hatofautiani  na
        punda aliyebeba mzigo wa vitabu asivyofaidika navyo. Mfano huu umebainishwa katika
        Qur’an kama ifuatavyo:


                 ُ َ َ  َ  ۡ  ۢ َ  َ ۡ  َ  ُ ۡ َ  َ  ۡ  َ َ  َ  َ  ُ  ۡ َ َ ُ َ  ٰ َ ۡ َّ  ْ ُ  ّ ُ َ  َّ  ُ َ َ
                                                          ۡ َّ
                لثم سئب ۚارافسأ لِمي رامِلٱ لثمك اهولِمي مل مث ةىرولتٱ اولِح نيِلٱ لثم
                        ِ
                                     ِ
                                            ِ
        FOR ONLINE READING ONLY
                                                                      ُ
                                َ    َّ  َ ۡ  َ  ۡ  ۡ َ  َ  ُ َّ َ َّ  َ  ْ َّ َ  َ  َّ  ۡ  َ  ۡ
                                                                 ٰ
                                    ٰ
                             ٥ينِمِلظلٱ موقلٱ يِدهي ل للٱو ِۚللٱ  ِ تيأَ ب اوبذك نيِلٱ ِموقلٱ
                                                                  ِ
                Mfano wa wale waliopewa Taurati kisha hawakuichukua (kwa kuitumia)
                ni kama punda anayebeba vitabu vikubwa vikubwa (bila ya kufaidika
                kwavyo).  Ni  mbaya  kabisa  mfano  wa  watu  waliokadhibisha  aya  za
                Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhalimu”
                (Al-Jumu’a, 62:5).
        Kwa mantiki hiyo, haitarajiwi kumuona Muislamu, anayejua madhara ya pombe, madawa

        ya  kulevya,  riba,  zinaa,  fitina,  kutukana,  dharau,  kukata  udugu,  ushirikina,  kutosali,
        kutowatii wazazi /walezi na walimu, wizi, ujambazi, muziki, kuvaa nusu uchi na mengine
        yaliyoharamishwa, kushiriki katika mchakato wa kufanikisha utekelezaji wa mambo hayo.


        Hivyo, kwa muktadha huo, elimu ni mchakato wa mabadiliko ya tabia, kutoka kwenye hali
        duni kiutendaji na kuelekea kwenye ufanisi. Pia, msomi aliyeelimika ni yule aliyebadilika
        tabia na mwenendo wake kutoka katika hali duni kiutendaji, kuelekea hali ya ufanisi,
        kutokana  na  ujuzi  alioupata  darasani  au  nje  ya  darasa,  vitabuni  au  katika  mazingira
        yaliyomzunguka. Ni katika maana hii Allah (S.W) anawafahamisha wanadamu kupitia

        Qur’an kwa kusema:

                        َ
                       ْ ْ ُ  ُ  َّ َ  َ َ َ  َّ  َ  َ  َ  َّ  َ  َ  َّ   َ ْ َ  ْ  َ  ْ ُ
                                             ُ ْ َ
                                                    َ
                                                             ُ ْ َ َ
                               ُ
                                                         َ
                       َ
                  ٩باللا ولوأ ركذتي امنِإ  نوملعي ل نيِلاو نوملعي نيِلا يوتسي له لق
                    ِ
                                                                         ِ
                “...Sema: Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?
                Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu.” (Az-Zumar, 39:9)
        Katika aya hiyo, Allah (S.W) anadhihirisha kuwa mjuzi na asiyejua hawawezi kuwa sawa
        kiutendaji na kitabia. Utendaji wa mtu mwenye ujuzi sahihi ni wenye mafanikio, na pia
        tabia yake huwa ni nyoofu, yenye kulingana na hadhi ya mwanadamu.
        Malengo ya elimu


        Ili kuona kwa upana zaidi malengo ya elimu, ni vema kutazama kwa ujumla mifumo ya
        elimu ya Ujamaa na Ubepari, kisha kuilinganisha na mfumo wa kipekee wa Uislamu.


                                                   3
   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18