Page 12 - EDK_F5
P. 12

SURA YA KWANZA                                                   ELIMU KATIKA UISLAMU


         Kazi ya 1 1

         Shirikiana na wanafunzi wenzako kuchunguza  kielelezo  namba  1 1 na kujadili
         mafunzo yatokanayo

        FOR ONLINE READING ONLY
        Maana na malengo ya elimu
        Sehemu hii, imeangazia tofauti za kimaana na kimalengo baina ya mfumo wa elimu wa
        Uislamu na mfumo wa elimu wa Ujamaa na Ubepari. Imeangaziwa mifumo ya elimu ya
        ujamaa na Ubepari, kwa sababu hii ndio mifumo mikubwa inayofuatwa na ulimwengu,
        hasa kutokana na ushawishi wa mataifa makubwa yanayobeba kampeni ya mifumo hiyo.

        Maana ya elimu


        Wanazuoni wameeleza maana ya elimu katika mitazamo mbalimbali, inayoakisi matumizi
        na mchakato wa upatikanaji  wake. Baadhi yao wameeleza  kuwa elimu  ni ujuzi na
        maarifa anayopata mwanafunzi kutoka kwa mwalimu. Wengine wameeleza kuwa elimu
        ni utaratibu wa mafunzo, maelekezo, maarifa, uwezo, maendeleo ya tabia na nguvu za
        kiakili zinazotokana na mafunzo hayo. Pia, wengine wameeleza kuwa elimu ni sanaa ya
        kutengeneza mwanadamu. Vilevile, wengine wameeleza kuwa elimu ni mabadiliko ya
        tabia, yanayotokana na maarifa aliyopata katika mchakato wa kujifunza. Kwa ujumla,
        elimu ni mabadiliko ya tabia yanayotokana na ujuzi.

        Wanazuoni wengi katika kueleza  maana ya elimu, wameishia kuihusisha elimu  na
        kujenga akili ya mwanadamu katika ulimwengu wa kivitu na kusahau roho. Wakati roho
        ndio msingi mkuu wa maadili katika jamii. Pia, mifumo ya elimu imezingatia hili kwa
        kuhakikisha mwanadamu anawezeshwa kupata elimu itakayomsaidia kupata maendeleo
        ya vitu bila kujali maadili yenye kunyanyua utu na heshima yake.

        Uislamu unaitazama elimu kuwa ni ujuzi ulioambatanishwa na utendaji. Ujuzi ambao
        unampatia msomaji msukumo wa kutenda kwa ufanisi, kwa kuzingatia maelekezo ya
        Allah (S.W), kutokana na kuimarika kwa mahusiano baina ya nafsi ya mwanadamu na
        dhati ya Allah (S.W). Maelekezo ya Allah (S.W) katika kutekeleza maisha ya kila siku,
        yanapatikana kupitia Qur’an na Sunnah ya Mtume Muhammad (S.A.W). Maelekezo hayo
        yanamwezesha mwanadamu kuwa bora katika jamii na kukuza utu, heshima na maadili
        yake.

        Elimu  haiishii  katika  kujua,  kunakotokana  na  kujifunza  au  kufundishwa,  bali  elimu
        hukamilika pale inapomwezesha mwenye kujua kutenda kwa ufanisi zaidi kuliko yule
        asiyejua. Aliyesoma bila kutafsiri alichokisoma katika matendo ya kila siku, ni sawa tu
        na asiyesoma, kwa sababu wote hawa hawainufaishi jamii. Katika hali hii, msomi huyu


                                                   2
   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17