Page 9 - EDK_F5
P. 9

DIBAJI

                                            Dibaji



                 itabu hiki cha somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa Kidato cha Tano ni  katika
                 mfululizo wa vitabu viwili  vya somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa shule za
        Ksekondari Kidato cha Tano na Sita. Kitabu hiki kimetayarishwa kwa kuzingatia
        FOR ONLINE READING ONLY
        muhtasari wa mwaka 2024 na kina sura kumi zifuatazo:

        1. Elimu katika Uislamu
        2. Itikadi katika Uislamu
        3. Nguzo za Imani
        4. Ithibati ya Qur’an

        5. Kufasiri Qur’an
        6. Ithibati ya Sunnah
        7. Utekelezaji wa nguzo za Uislamu
        8. Uislamu na Mifumo ya Maisha

        9. Historia katika Uislamu
        10. Historia ya Uislamu
        Sura hizo zimekidhi  na kutosheleza  umahiri  mkuu, umahiri  mahsusi na shughuli za
        ujifunzaji  kwa Kidato cha Tano kama ilivyo katika muhtasari.

        Aidha, kitabu hiki kimetayarishwa kwa kuzingatia mbinu za kumuwezesha mwanafunzi
        kujifunza  kwa  kutenda  zaidi  akiwa  darasani  na  nje  ya darasa.  Hivyo, maudhui
        yamewasilishwa kwa njia ya matini, kazi za kufanya na vielelezo  ili kumvutia na
        kumshajiisha mwanafunzi kukisoma. Pia, kitabu kina kazi na mazoezi ya kutosha ndani na
        mwishoni mwa kila sura, ili kumuwezesha mwanafunzi aendelee kujipima na kujiimarisha
        katika kukuza umahiri uliokusudiwa. Kwa hiyo, mwanafunzi anapaswa kufanya mazoezi
        na kazi zote zilizomo ndani ya kitabu hiki, pamoja na kazi nyingine atakazopewa na
        mwalimu zitakazomuandaa vema kufaulu mtihani wa  Taifa.

        Upekee wa Kitabu hiki ni kuwa maudhui na hoja zilizomo, zimetayarishwa kwa mtindo
        mpya, licha ya kuwa huu ni mwendelezo wa ngazi ya Sekondari ya chini; Kidato cha
        Kwanza hadi cha Nne. Kitabu hiki ni cha kiuchambuzi zaidi, ili kumwezesha mhitimu
        kuwa mtendaji, mdadisi, mwenye upeo wa kutosha wa Elimu ya Dini ya Kiislamu na
        mjengaji wa hoja. Hoja zimefafanuliwa kwa kiwango kinachoendana na Kidato cha Tano
        na Sita  ambapo baadhi ya hoja zimewekwa kwa makundi  sio mojamoja kama ilivyokuwa
        katika Sekondari ya chini. Mfano hoja zinazothibitisha kuwa Qur’an ni maneno ya Allah
        (S.W) zimewekwa katika makundi manne.





                                                  vii
   4   5   6   7   8   9   10   11   12   13   14