Page 7 - Jiografia_Mazingira
P. 7

Utangulizi


          Kitabu cha Jiografia na Mazingira kimetayarishwa kwa kuzingatia

          muhtasari wa somo la Jiografia na Mazingira elimu ya msingi Darasa
        FOR ONLINE READING ONLY
          la III - VI uliotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
          mwaka 2023. Baadhi ya maudhui ya kitabu hiki yamechukuliwa
          kutoka katika vitabu vya Maarifa ya Jamii Darasa la Tatu, la Nne
          na la Tano vilivyochapishwa mwaka 2018 kwa kuzingatia muhtasari

          wa mwaka 2016. Kitabu hiki kina sura nne, ambazo ni Dhana ya
          ramani, Pande Kuu za Dunia, Uchoraji wa ramani sahili na Matumizi
          ya ramani. Kwa kujifunza maudhui ya kitabu hiki utakuza maarifa,

          stadi na mwelekeo katika kuchora, kusoma na kutafsiri ramani.
          Maudhui ya kitabu hiki yamewasilishwa kwa njia ya matini, kazi za

          kufanya, michoro na ramani mbalimbali ili kukuwezesha kujenga
          umahiri uliokusudiwa katika kila sura. Kila sura ina mazoezi ya
          kutosha yatakayokuwezesha kupima uelewa wako kuhusu maudhui
          husika. Hivyo, unashauriwa kufanya kazi na mazoezi yote yaliyopo

          katika kitabu hiki pamoja na kazi zingine utakazopewa na mwalimu
          ili kujenga umahiri uliokusudiwa.





          Jifunze zaidi kupitia Maktaba Mtandao https://ol.tie.go.tz au ol.tie.
          go.tz



















                                                         Taasisi ya Elimu Tanzania




                                                  vi



                                                                                          31/10/2024   19:17
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   6
   JIOGRAFIA NA MAZINGIRA DARASA LA 4.indd   6                                            31/10/2024   19:17
   2   3   4   5   6   7   8   9   10   11   12