Page 28 - Sanaa_Michezo_Drs_4
P. 28

(iii)  Karatasi;

                   (iv) Kifutio;

                   (v)  Meza na kiti;

                   (vi) Kibao cha kuchorea; na
        FOR ONLINE READING ONLY
                   (vii) Kibanio cha kubania karatasi

          Kanuni za uchoraji wa picha njiti


          Ili kuchora picha njiti, kanuni zifuatazo ni muhimu kuzingatiwa:

          1.  Picha njiti ichorwe kwa kuzingatia ujumbe husika;

          2.  Fikiria  wazo  la  kitu utakachochora  au andaa  kitu halisi
               kitakachochorwa;

          3.  Zingatia matumizi mbalimbali ya mistari ili kupata uhalisia wa
               jambo;

          4.  Anza kuchora kwa kutumia mistari myepesi;


          5.  Tumia kifutio kwa uangalifu ili usichafue mchoro; na

          6.  Usitumie kalamu ya wino kuchorea picha katika hatua hii.

          Hatua za kuzingatia katika kuchora picha njiti

          Katika kuchora picha njiti, zipo hatua ambazo unatakiwa kuzizingatia
          ili picha yako ilete maana. Hatua hizo ni:

              (a)  Chagua au buni vitu unavyotaka kuchora;


              (b)  Andaa karatasi na penseli ya kuchorea;

              (c)  Anza kuchora picha njiti kwa kutumia mistari myepesi;

              (d)  Rekebisha  kama kuna sehemu ambayo umekosea  kwa
                    kutumia kifutio;

              (e)  Koleza mistari baada ya kuwa umepata umbo sahihi; na

              (f)  Ondoa mistari isiyotakiwa pamoja na uchafu uliosababishwa
                    na ufutio.




                                                 21




                                                                                          19/10/2024   16:35
   SANAA NA MICHEZO BALANCING.indd   21
   SANAA NA MICHEZO BALANCING.indd   21                                                   19/10/2024   16:35
   23   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33