Page 29 - Sanaa_Michezo_Drs_4
        P. 29
     Hatua za kuchora picha njiti ya umbo la binadamu
                   (i)  Fikiria uelekeo wa umbo la binadamu. Chagua upande
                        umbo litaelekea kama ni kulia au kushoto;
                   (ii)  Chora duara la kichwa.  Anza na duara dogo juu ya
        FOR ONLINE READING ONLY
                        karatasi yako. Hili litakuwa kichwa cha picha njiti ya
                        umbo la binadamu;
                   (iii)  Chora shingo na  mabega.  Chora mstari wa msalaba
                        unaoungana na kichwa;
                   (iv) Chora  kiwiliwili  (kifua na tumbo). Chora mstari wima
                        moja kwa moja kutoka kichwani.  Mstari huu utakuwa
                        umbile la kiwiliwili la picha njiti ya umbo la binadamu;
                   (v)  Chora mikono. Chora mistari miwili inayotoka sehemu
                        ya  juu ya  mstari  wa kiwiliwili.  Mistari hii inawakilisha
                        mikono. Unaweza kuongeza miduara midogo mwishoni
                        kwa ajili ya viganja;
                   (vi) Chora miguu. Chora mistari miwili  inayotoka  chini
                        ya mstari wa msalaba.  Mistari  hii  inaonesha  miguu.
                        Unaweza kuongeza miduara midogo mwishoni kwa ajili
                        ya kuonesha nyayo za miguu;
                   (vii) Koleza mistari. Koleza mistari ya picha yako kwa kutumia
                        penseli, kama inavyoonekana  katika Kielelezo namba
                        2.
                                                 22
                                                                                          19/10/2024   16:35
   SANAA NA MICHEZO BALANCING.indd   22                                                   19/10/2024   16:35
   SANAA NA MICHEZO BALANCING.indd   22
     	
