Page 36 - SayansiStd4
P. 36

Sura ya Pili






                                             Magonjwa
          FOR ONLINE READING ONLY




                Utangulizi

                Magonjwa huathiri afya za watu. Katika sura hii, utajifunza
                kuhusu magonjwa  ya binadamu. Aidha, utajifunza njia za

                maambukizi, visababishi na namna ya kudhibiti na kujikinga
                na magonjwa. Vilevile, utajifunza hatua za ukuaji wa baadhi
                ya wadudu  wanaoeneza  magonjwa  mbalimbali.  Umahiri
                utakaoujenga utakuwezesha kudhibiti magonjwa mbalimbali.

                Vilevile, kujikinga na kuwakinga wengine dhidi ya magonjwa.





                                      Madhara ya  magonjwa katika afya ya
                              Fikiri
                                      binadamu





              Dhana ya magonjwa


              Ugonjwa  ni  hali  ambayo  inadhoofisha  afya  na  hivyo  kuathiri
              utendaji  wa kawaida wa mwili. Magonjwa mengi hutokana
              na vimelea au vijidudu mbalimbali vilivyopo katika mazingira
              yetu. Vimelea hivyo huishi katika hewa, udongo, maji, chakula

              kisicho salama na kwenye majimaji ya miili ya wanyama kama
              vile damu. Vimelea hivyo huingia mwilini kupitia njia mbalimbali
              kama vile kula chakula chenye  vimelea,  kuvuta hewa  na
              kugusana. Aidha, baadhi ya magonjwa hayatokani na vimelea.

              Magonjwa hayo ni kama vile magonjwa ya kurithi.




                                                   29




                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   29
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   29                                   14/01/2025   18:39
   31   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41