Page 39 - SayansiStd4
P. 39

(d)  Viungo vya mwili kukosa nguvu;

              (e)  Kutapika; na

              (f)  Kupoteza hamu ya kula.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Namna ya kuzuia malaria
              Ugonjwa wa malaria huzuiwa kwa kuharibu mazalia ya mbu.

              Mazalia ya mbu ni kama vile kwenye vichaka, nyasi ndefu
              na maji yaliyotuama kwenye vidimbwi. Pia, matairi, vifuu vya
              nazi na makopo yaliyohifadhi  maji yanaweza kuwa mazalia

              ya mbu. Maji yaliyotuama  yanaweza  kumwagiwa  mafuta ya
              taa au viuadudu ili kuua mazalia ya mbu. Pia, vifuu vya nazi
              na vifaa vingine vyenye mazalia vichomwe moto. Aidha, njia
              za kujikinga na malaria ni kutumia  vyandarua  vyenye  dawa

              maalumu wakati wa kulala na kutumia dawa za kufukuza au
              kuua mbu.  Njia nyingine  ya kujikinga  na malaria ni kuweka
              nyavu katika madirisha ya nyumba ili kuzuia mbu kuingia. Mtu
              anapohisi dalili za malaria anapaswa kuwahi hospitali au katika

              kituo cha afya ili apate uchunguzi na tiba sahihi.


               Zoezi namba 2

               1.  Taja dalili nne za ugonjwa wa malaria.

               2.  Eleza umuhimu wa kulala kwenye chandarua.


               3.  Fafanua namna mtu anavyoweza kuambukizwa malaria.


               4.  Je, unawezaje kujikinga wewe na familia yako dhidi ya
                     malaria?



              Kipindupindu

              Kipindupindu  ni ugonjwa unaosababishwa  na bakteria.
              Kipindupindu  kinaenezwa kwa kula chakula au kunywa maji

              yenye vimelea vya kipindupindu. Pia, ugonjwa huu huenezwa



                                                   32



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   32                                   14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   32
   34   35   36   37   38   39   40   41   42   43   44