Page 41 - SayansiStd4
P. 41

kutumia vyoo kwa usahihi.  Tunapaswa  kunawa mikono kwa
              maji safi yanayotiririka na sabuni baada ya kutoka chooni na
              kabla ya kula chakula. Mtu akipatwa na kipindupindu apelekwe
              hospitali  haraka au katika kituo maalumu kilichotengwa  kwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              ajili ya ugonjwa huo.


               Zoezi namba 3

               1.  Eleza jinsi ugonjwa wa kipindupindu unavyoweza kuenea.


               2.  Unawezaje kumtambua mtu mwenye kipindupindu?

               3.  Ni mambo gani  ya kufanya ili kuzuia kipindupindu?


               4.  Eleza kwa nini ni muhimu kunawa mikono yako kwa
                     sabuni na maji safi yanayotiririka baada ya kutumia choo.



              Tetekuwanga

              Tetekuwanga ni ugonjwa unaosababishwa na virusi. Ugonjwa

              huu huambukizwa kwa njia ya kugusana mwili na mtu aliye na
              tetekuwanga. Pia, huweza kuambukizwa kwa kuvaliana nguo
              na mtu aliye na tetekuwanga.


              Dalili za tetekuwanga

              Dalili  za tetekuwanga  ni pamoja
              na homa kali na kuumwa kichwa.

              Vilevile,     kutokwa       na     vipele
              vinavyowasha ambavyo hubadilika
              kuwa malengelenge  yanayotoa
              usaha       au     majimaji.      Wakati
              mwingine  ugonjwa  huu  huacha

              makovu ya kudumu kwenye ngozi.
              Kielelezo namba 3  kinaonesha
              mgonjwa wa tetekuwanga.                             Kielelezo namba 3:
                                                               Mgonjwa wa tetekuwanga



                                                   34



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   34
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   34                                   14/01/2025   18:39
   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46