Page 37 - SayansiStd4
P. 37

Zoezi namba 1

               1.  Bainisha  sehemu mbalimbali  ambapo vimelea vya
                     magonjwa hupatikana.

          FOR ONLINE READING ONLY
               2.  Eleza njia mbalimbali  ambazo vimelea vya magonjwa
                     vinaweza kuingia mwilini mwa binadamu.


               3.  Taja magonjwa  yoyote matatu unayoyafahamu  katika
                     mazingira yako?




              Aina za magonjwa

              Kuna aina mbalimbali za magonjwa   yanayoathiri  utendaji
              wa kawaida wa mwili wa binadamu.  Magonjwa hayo

              yamegawanyika  katika makundi  makuu mawili  ambayo  ni
              magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza.






                Kazi ya kufanya namba 1


               1.  Tumia maktaba, matini mtandao  au vyanzo vingine
                     kutafuta taarifa kuhusu magonjwa  ya kuambukiza  na

                     yasiyo ya kuambukiza.

               2.  Orodhesha mifano mitano kwa kila kundi la magonjwa
                     uliyoyabaini.



              Magonjwa ya kuambukiza


              Magonjwa  ya kuambukiza  ni magonjwa  yanayoenezwa
              kutoka kwa  mtu  mmoja kwenda kwa mwingine. Magonjwa
              hayo husababishwa na vimelea. Mfano wa vimelea hivyo ni
              bakteria, na virusi. Magonjwa hayo ni kama vile kipindupindu,
              tetekuwanga, kifua kikuu, homa ya ini na Ugonjwa wa Virusi vya




                                                   30



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   30
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   30                                   14/01/2025   18:39
   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41   42