Page 40 - SayansiStd4
P. 40

na nzi. Nzi anaweza kubeba vimelea kutoka kwenye matapishi
              au kinyesi chenye vimelea kwenda kwenye chakula au maji.
              Kielelezo namba 2  kinaonesha  uenezwaji wa ugonjwa wa
              kipindupindu.
          FOR ONLINE READING ONLY
               Nzi aliyebeba vimelea
               vya ugonjwa akielekea

               kwenye chakula










              Kinyesi chenye
              vimelea vya
              ugonjwa wa                                                  Mtu

              kipindupindu                                                aliyeambukizwa
                                                                          ugonjwa wa
                                                                          kipindupindu

                    Kielelezo namba 2: Uenezwaji wa ugonjwa wa kipindupindu

              Dalili za kipindupindu

              Zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kipindupindu:


              (a)  Kuharisha na kutapika mfululizo;

              (b)  Kutoa kinyesi chenye rangi kama ya maji yaliyosafishiwa
                   mchele;

              (c)  Mkojo kuwa na rangi ya manjano; na


              (d)  Kulegea mwili na kuishiwa nguvu.

              Namna ya kuzuia kipindupindu

              Tunapaswa  kuishi  katika  mazingira  safi  na  kudumisha  usafi.
              Tunashauriwa  kula  chakula  na  kunywa  maji  safi  na  salama.

              Aidha, ni muhimu kutumia choo wakati wa kujisaidia.  Pia,


                                                   33




                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   33                                   14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   33
   35   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45